UTAMJUAJE MTU ALIYEATHIRIKA NA UCHAWI AU MAJINI?.


1.  Kuumwa kichwa upande mmoja,meno,mgongo,kiuno na kubanwa kifua.
2.  Kuumwa tumbo chini ya kitovu hii ni kwa akinamama.
3.  Moyo kwenda mbio na kushtuka bila asbabu.
4.  Kushika moto mwili hasa miguu pmj na ganzi na maumivu makali.
5.  Kizunguzungu mara kwa mara.
6.  Kuumwa tumbo sana kwa akinamama wakati wa period pmj na kutoa damu nyingi au chache sana.
7.  Kupata maumivu makali wakati wa jimai kwa akinamama na kukosa hamu ya tendo hilo au kulichukia kabithaaaa.
8.  Kutembelewa na vitu mwilini.
9.  Kutingishika,kutetemeka sana na kulia bila sababu ikiwemo na hasira sana.
10.  Kuhisi uzito wa mwili kana kwamba umebeba mzigo mzito.
11.  Chuki ndani ya ndoa kutamani kuachwa au kuacha bila asbabu.
12.  Maneno machafu kwa mwenza na punde tyuu majuto mjukuu.
13.  Kufungika hedhi bila sababu na kutoshika ujauzito bila sababu za msingi.
14.  Kuota umjauzito,unazaa,unanyonyesha na unabeba watoto.
15.  Kujaa kitumbo ndiiii bila ujauzito na kuchezacheza kitu tumboni bila ya ujauzito.
16.  Kuharibika mimba baada ya kuota unafanya vituuuuz na mtu atishae au hata umjuae au usiyomjua.
17.  Kuyeyuka na kuharibika mimba bila sababu za msingi.
18.  Ndoto za jimai mara kwa mara.
19.  Kuwa na hamu sana ya mambo yetu yaleeeeeee uwapo peke yako lkn ukutanapo na mwenza hamu hiyooooo ishasepa na kwa mume hupotelewa na nguvu ghafla.
20.  Kuvurugika mipango ya kuoa au kuolewa mara kwa mara.
21.  Kuhisi unaingiliwa au kuingilia babaweeeee hii sio ndotonivyoooooo uvitambue babaaaaaa.
22.  Kutopenda ibadah lkn maasi unayapa mahabba mazitooo.
23.  Hasira,uvivu pmj na hofu bila sababu.
24.  Kuhisi kusimamiwa na mtu mbele yako,nyuma,pembeni na hata ulalapo na kuwa na hofu sana juu ya hilo.
25.  Kukosa usingizi au usingizi mzito mpk swalat subhi ikakupita.
26.  Usomapo Qur-an au kusikiliza hotuba ya ijumaa hupata usingizi a.k.a kusinziasinzia lkn usomapo magazeti au mazungumzo mengine usingizi hauji ng'oooo.
27.  Tamaa kupita kiasi na kujihisi ni mtu wa thamani sana kinyume na ulivyo.
28.  M/mke kupenda kujiremba awapo nje ya nyumba yake lkn akiwa ndani kwake huwa hajirembi na km ana mume basi hubaki kumuachia harufu mbaya mumewe. loh wanawake nyiyeeee loh hebu jirembeni mkiwa ndani ili sisi waume zenu tujihisi kupendwa nasi tukazidisha upendo.
29.  Kupenda vitu vya upuuzi km vile miziki,porojo,udaku,vipindi vya TV visivyo na maana au redio.
30.  Kuota ndoto za vitisho km vile wanyama wakali,au unafanyiwa uadui au unazingirwa na maji,kifo,jeneza,unatumbukia shimoni na unapaa hewani wala mbawa hauna.
31.  Kuota ibada zisizo na mwelekeo.
32.  Kulia,kucheka na kupiga kelele usingizini a.k.a Jinamizi.
33.  Kuchanganyikiwa ndani ya swala pmj na kuyumba na kusinzia usiisahauvyooo.
34.  Kuota mtu mfu au unaelezwa jambo ndotoni na ikiwa yote ni kweli hali hauna Uchamungu na hivyo.
35.  Kuota watu watishao.
36.  Kuota sana nyumba za ibada (misikiti)hali wewe si mtu wa ibada.
37.  Kuota unafanya mashauri na watuwafu a.k.a Mizimuuu.
38.  Kuota unafanyiwa shughuli zote za mazishi au unamfanyia mwenzio.
39.  Kuota unaingiliwa au unaingilia kinyume na maumbile a.k.a Liwatwi.
40.  Kushtukashtuka mara kwa mara usingizini.
41.  Kuibiwa pesa hata uzifungie waaaaapi vileeeee a.k.a Chumaulete.
Haya ndg zangu hizo ndio dalili 41 nilizosema nitawaekea na zipo nyingi zote hizo zinaashiria mtu kusumbuliwa na shetani wa kijini (wachawi) na mtu sio lzm awe nazo zote